TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24

TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24 - FINANCIAL-24, we has prepared this article well for you to read and retrieve information in it. Okay, happy reading.

TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24

Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imeagana na Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing katika hafla fupi ambayo imefanyika katika hoteli ya Serena iliyopo Dar es Salaam. 

Akizungumza katika hafla ya kumuaga, Mwenyekiti wa TPSF, Dk. Reginald Mengi alimshukuru Dk. Youqing kwa mambo yote ambayo ameyafanya akiwa balozi wa China nchini na kumuomba kuendelea kushirikiana na Tanzania hata atakaporejea China. “Muda mwingine nashindwa kujua kama unaiwakilisha China au Tanzania umekuwa na matendo mema kwa Tanzania kwa kipindi chote ambacho umefanya kazi nchini umekuwa daraja kubwa la kuunganisha China na Tanzania, “Wote tunajua umuhimu wa biashara ya Tanzanania na China ilivyo kubwa na mambo mambo mengi uliyoyafanya yalifanikiwa, jambo ambalo tunaweza kusema ni tutakukumbuka sana,” alisema Dk. Mengi. 

Kwa upande wa Dkt. Lu Youqing aliishukuru TPSF kwa ushirikiano waliomba kwa kipindi chote ambacho alikuwa akifanyakazi nchini na kuahidi kuwa hata atakaporudi China ataendelea kushirikiana nao. “Tumeishi vizuri kwa kipindi nilichokuwa hapa niwaahidi kuwa nitarudi tena Tanzania nikiwa kama mfanyabiashara na siku moja ninapenda kuwa mwanachama wa TPSF, kuweni huru kuja hata China kujifunza namna China tunafanya biashara,” alisema Dkt. Youqing.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi akisalimia na Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi na Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing wakiingia katika ukumbi wa mikutano wa Kivukoni uliopo katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi akizungumza katika hafla ya kumuaga Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing.

Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing akizungumza katika hafla ya kumuaga baada ya muda wake wa kufanya kazi nchini kuisha.




Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi na Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing wakiwa na viongozi wengine wa TPSF walioshiriki hafla ya kumuaga Balozi Youqing.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi na Balozi wa China aliyemaliza muda wake chini Dkt. Lu Youqing wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa TPSF.

This is the article TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24 this time, hopefully can benefit for you all. well, see you in other article post.

Title : TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24
link : TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24

0 Response to "TPSF YAMUAGA BALOZI WA CHINA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI - FINANCIAL-24"

Post a Comment